DOAJ Open Access 2023

Uibukaji wa U-Nigeria katika Tasnia ya Muziki wa Kizazi Kipya Nchini Tanzania: Masuala Muhimu ya Kuzingatia

Gervas A Kasiga

Abstrak

Imebainika kuwa tasnia ya muziki wa kizazi kipya wa Kiswahili nchini Tanzania imetekwa na utamaduni wa nje hususani wa Kinigeria (Mrikaria, 2007; Kasiga, 2022). Athari zake zimebainika katika vipengele kadhaa vya kibunifu (Kasiga, 2021). Pia, misukumo mbalimbali inayowasukuma wasanii kutumia U-Nigeria imebainishwa (Kasiga, 2022). Kimsingi, hali hii inatishia utambulisho wa Kitanzania katika sanaa. Hivyo, makala hii imetoa mapendekezo ya kiuboreshaji dhidi ya U-Nigeria katika video za nyimbo za muziki wa kizazi kipya wa Kiswahili nchini Tanzania. Mapendekezo yaliyotolewa yamehusisha: kufanyika uwekezaji wa muziki wa asili wa Kitanzania, kufanyika kwa usimamizi maalumu katika vyombo vya habari, kuwepo kwa sheria na kanuni za kulinda uasili wa muziki wa kizazi kipya, na uanzishwaji wa semina, warsha pamoja na madarasa maalumu kwa wasanii. Isitoshe, makala imependekeza kuwepo kwa agenda mahususi ya kitaifa kujenga uzalendo, kumakinikia mitindo ya sanaa za Kitanzania katika utengenezaji wa muziki, kuharakisha upatikanaji wa vazi la taifa, kuanzishwa kwa vipindi vya uchambuzi wa nyimbo, na wasanii kushawishiwa kutumia mandhari ya Kitanzania katika video zao. Zaidi, imependekezwa kuanzishwa kwa matamasha na tuzo za muziki, asasi za elimu kutengeneza mitaala ya biashara, lugha ya Kiswahili, na utamaduni wa Kitanzania, na kuwe na muumano kati ya biashara, utamaduni na teknolojia.

Penulis (1)

G

Gervas A Kasiga

Format Sitasi

Kasiga, G.A. (2023). Uibukaji wa U-Nigeria katika Tasnia ya Muziki wa Kizazi Kipya Nchini Tanzania: Masuala Muhimu ya Kuzingatia. https://doi.org/10.58721/jkal.v1i1.93

Akses Cepat

PDF tidak tersedia langsung

Cek di sumber asli →
Lihat di Sumber doi.org/10.58721/jkal.v1i1.93
Informasi Jurnal
Tahun Terbit
2023
Sumber Database
DOAJ
DOI
10.58721/jkal.v1i1.93
Akses
Open Access ✓